• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mwenyekiti wa Halmashauri amewataka watumishi kufanya kazi kwa kushirikiana

Posted on: July 27th, 2023

Watumishi wa Halmashauri ya Mji Newala wametakiwa kufanya kazi zao kwa kushirikiana wao kwa kwao pamoja na viongozi wengine ili kurahisisha lengo la serikali la kuwafikishia wananchi maendeleo kwa haraka.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Yusuph Kateule Jumatano Julai 26,2023 wakati anafunga kikao cha kamati ya fedha robo ya nne 2022/2023 na kumkaribisha Mkurugenzi mpya wa halmashauri hiyo pamoja na Katibu Tawala mpya wa wilaya ya Newala.

Mheshimiwa Katule akiwakaribisha viongozi hao amesema watumishi wa serikali kila mmoja anapaswa kutekeleza majukumu yake kwa weledi, uwazi na ushirikiano hali itakayopelekea wananchi kupata huduma bora kutoka kwenye vitengo na idara za serikali.

“Nikushukuru sana Katibu Tawala nikukaribishe Newala pia nikushukuru Mkurugenzi karibu sana sisi tunamatumaini na wewe, watumishi jitahidini kuweka mambo vizuri, muwe na ushirikiano ninyi kwa ninyi na kuweni wawazi ili tuwatumikie wananchi wetu vizuri”. Alieleza Mheshimiwa Kateule

Kwa upande wake Katibu Tawala mpya wa Wilaya ya Newala Ndg. Thomas Safari amesema hakuna njia ya mkato ya kufikia mafanikio katika utendajikazi hasa wa taasisi kama halmashauri ni lazima kuwe uwajibikaji wa pamoja kwa kuwa lengo la watumishi wote ni moja.

“Mfano sasahivi mna hivi vishikwambi kuna mambo ya kidigitali lakini je ? ulipoona kasoro kwenye taarifa kama ya ukaguzi ulichukua hatua gani kumuona mkaguzi au kumuambia mwenzako amuone mkaguzi ili kuweka sawa mambo yake.. lazima mshirikiane”. Alifafanua katibu Tawala huyo.

Hata hivyo Katibu Tawala Safari amewataka watumishi kupendana, kushauriana na kukosoana kwa nia njema pale inapojitokeza mwingine amekosea au kuonesha udhaifu katika utendaji jambo ambalo litasaidia kuimarisha sifa ya mtumishi na huduma zinazotolewa na halmashauri.

Akizungumza kwa mara ya kwanza katika kikao hicho Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndg. Geofrey Nnauye ameahidi kutoa ushirikiano katika kutekeleza majukumu na kuwasisitiza watumishi kusimamia uwazi na kujituma wakati wa kutekeleza majukumu yao.

Aidha Nnauye ametaka kila mmoja asimamae kwenye nafasi yake aliyoaminiwa na serikali kutimiza wajibu wake wakiutumishi kwa uaminifu ili kujiweka salama na kuondokana dosari za kunyooshewa vidole au kutiliwa shaka.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa