• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Nguvu ya pamoja yaitajika kuondoa utapiamlo Newala mji

Posted on: August 21st, 2019

Jamii imeshauriwa kuweka kipaumbele katika kupambana na tatizo la utapiamlo kuanzia pale mama anapopata ujauzito kwani tatizo hilo bado lipo na athari zake ni kubwa na za muda mrefu.

Rai hiyo imetolewa na kaimu mganga mkuu wa halmashauri ya mji Newala Dkt. Athanase Emmanuel ambaye alikua katibu kwenye kikao cha kamati ya lishe cha robo ya nne 2018/2019, kilichofanyika jana 20/08/2018 ambapo amesema elimu zaidi inahitajika ili jamii iondokane na tatizo hilo.

Amesema matatizo kama ya udumavu wa akili wakati mwingine yanasababishwa na utapiamlo, kwa watoto wadogo kukosa matone ya vitamin A, chanjo na lishe bora hivyo ni wakati muafaka wa kuchukua hatua ili kutengeneza Taifa imara kuelekea uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake Afisa elimu sekondari Mwl. Athuman Salum, akimuakilisha mwenyekiti wa kamati hiyo, amesisitiza na kushauri kuwa elimu ya utapiamlo kuwa ajenda ya kudumu kwenye vikao mbalimbali vya vijiji kata na kamati ya huduma za jamii ili watu wawe na uelewa ya kutosha juu ya tatizo hilo.

Hata hivyo ameitaka kamati hiyo kuhakikisha inazuia uuzaji wa chunvi zisizo na madini joto pamoja na kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua wafanyabiashara wanaouza bidhaa za chakula na viuatifilu katika maduka yao kwani si salama kwa watumiaji.

Naye Afisa lishe wa halmashauri hiyo Bw. Enos Kuzenza amesema lipo tatizo la watu kuendelea kutumia chunvi isiyo na madini joto hasa chunvi ya mawe kwa kuwa inaweza kusababisha matatizo ya kuharibika mimba kwa mama mjamzito au utindio wa ubongo kwa mtoto atakayezaliwa.

Kuzenza amesema kwenye robo hii ya nne, yapo mafanikio yaliyopatikana ikiwa pamoja na kutoa matone ya vitamin A kwa watoto 11,650 wenye umri wa miezi 6 na chini ya miaka 5 sawa na asilimia 96.7% na dawa za kutibu minyoo kwa watoto 10,102 wa miezi 12 na chini ya miaka 5 sawa na asilimia 97.4% ya malengo kusudiwa.

Aidha ameeleza kuwa wajazito 2414 kati ya 2868 waliohudhuria waliohudhuria kliniki walipatiwa dawa za kuongeza wekundu wa damu (FEFO), watoto 72 wamepatiwa matibabu ya utapiamlo mkali pamoja na vituo vyote 14 vya afya vimepatiwa chakula dawa na vifaa vya kuwatambua watoto wenye utapiamlo mkali.



Matangazo

  • TANGAZO MIKOPO YA VIWANJA NA MATOFALI October 12, 2021
  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji ataka ulinzi wa watoto kwa kufunika visima vya maji

    May 11, 2023
  • Idara ya Afya yatakiwa kusimamia mpango wa Taifa wa udhibiti malaria

    May 10, 2023
  • Viongozi wa kata na vijiji wanatakiwa kusimamia upatikanaji wa chakula shuleni

    May 09, 2023
  • Wananchi wa Tarafa ya Mkunya waishukuru Serikali kwa kuwaboreshea huduma za afya

    May 04, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa