• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Wananchi wa Tarafa ya Mkunya waishukuru Serikali kwa kuwaboreshea huduma za afya

Posted on: May 4th, 2023

Wananchi wa Tarafa ya Mkunya Halmashauri ya Mji Newala mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwatatulia changamoto ya upatikanaji wa huduma za Afya kwa kuwajengea na kuwapatia wahudumu katika kituo cha afya Mkunya.

Wakiongea kwa nyakati tofauti hivi karibuni wakazi hao wamesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anafanyakazi kubwa ya kuwatumikia wananchi na wanamshukuru kwa kuwaboreshea huduma za afya.

Mzee Abdallah Mkamate (75) mkazi wa kijiji cha Pachoto amesema ni furaha kwa upande wake kituo hicho kuwa karibu kwa kuwa awali walikua wanapata shida kwenda mbali kufuata huduma katika hospitali za Newala, Ndanda, Nyangao , Luagala, Mkomaindo na Lindi.

 Hata amempongeza Mhe. Dkt. Rais na mtangulizi wake Dkt. Magufuli kwa uongozi wao “sisi zamani tulikua tunakwenda huko kutibiwa haumjui mtu, haujui pakufikia na ukilazwa ni tatizo nani atakupa msaada au hata daktari hakujui kama hauna hela hauwezi hata kuomba, hapa unaweza hata ukajieleza kesho ukaleta pesa, kwahiyo uongozi wa sasa ni nzuri” Alieleza Mzee Mkamate.

Bi. Zena Mtave mkazi wa Mcholiwa Godauni amesema kwa sasa huduma za afya kwa wanawake na watoto zimeimarika tofauti na kipindi cha nyuma ambapo kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wajawazito kupoteza maisha hasa pale inapojitokeza changamoto wakati wa kujifungua kutokana umbali wa kwenda kupata huduma za uhakika

 ‘Siku hizi kwakweli tunafurahi sisi wanawake tunapimwa, tunalazwa hapa hapa zamani tulikua tunataabika kwenda Newala hospitali ni mbali na kuna gharama za usafiri pikipiki yaani tulikua tunashindwa, naipongeza serikali, Mama Samia na wote wanao husika”. Alieleza Bi. Zena

Nae Bi. Aisha Athuman Mkazi wa kijiji cha matokeo amesema wanafurahia huduma wanazopata toka kwa wahudumu hasa huduma za watoto na upatikanaji wa dawa kutokana na utaratibu nzuri uliopo uliowekwa huku akiiomba serikali kuongeza dawa kwa kuwa zinazopatikana huwa zinaisha mapema.

Kwa upande wake Bw. Shaibu Abdallah mkazi wa kijiji cha Pachoto ameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa Afya za wananchi wa Tarafa ya Mkunya ambao mwanzo walifuata huduma hizo mbali na kuiomba kuwaboreshea katika kuongeza wataalamu na vifaa tiba.

Kituo Cha Afya Mkunya kimejengwa kwa fedha za Serikali kuu kwa gharama ya shilingi milioni 600 na kimekuwa mkombozi kwa wakazi wa tarafa hiyo na kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali kuu ya Newala.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa